Maandamano ya wanafunzi yachacha Afrika Kusini
Aidha maafisa wa polisi walilazimika kufyatua risasi za plastiki na mabomu ya kutoa machozi ilikuwatanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana katika miji mikuu ya Port Elizabeth na Durban.
Waziri wa elimu aliwaahidi wanafunzi kuwa nyongeza hiyo haitapita asilimia 6% mwakani 2016 lakini hata hilo wanafunzi wamekataa.
Maandamano yanaendelea ya kupinga nyongeza hiyo ya karo.
Waandamanaji wanasema nyongeza ya karo itawafanya wanafunzi weusi kutoka familia maskini kukosa elimu kabisa.
Kufikia sasa vyuo vikuu 10 vimeathirika na makabiliano hayo baada ya muungano wa wanafunzi South African Students Congress (Sasco) kuitisha mgomo wa kitaifa.
Wanafunzi kadhaa wa chuo kikuu cha Cape Town (UCT) waliokamatwa watafikishwa mahakamani juma lijalo.
Wanafunzi wanataka masomo ya chuo kikuu iwe ya bure kama ilivyoahidiwa na serikali ya ANC ilipochukua hatamu ya uongozi baada ya uhuru wa taifa hilo.
Waziri wa elimu Blade Nzimande amesema kuwa kwa sasa serikali hiyo haina uwezo wa kulipia wanafunzi wote karo ya shule.
Maandamano haya yaliaoanzia shuo kikuu cha Johannesburg Witwatersrand sasa yameenea hadi chuo kikuu cha Cape Town, Rhodes , Stellenbosch , Fort Hare , chuo kikuu cha Free State na Cape Peninsula University of Technology.
Aidha ripoti zinaashiria kuwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Pretoria nao wameanza kuandamana. PICHA CHAFU ZA WANAFUNZI WAKIFANYA UCHAFU ZAVUJA FACEBOOK SEE PHOTOS BELOW =>AdvertisementKAMA HUJAONAILE VIDEO CHAFU YA ZARI THE BOSS LADY ILIYOVUJA BOFYA HAPO CHINI=> Advertisement
Post a Comment