FIGO ZA BINADAMU KUTENGENEZWA HUKO JAPAN SOMA USTAAJABU
Watafiti hao kutoka Japan waliepuka matatizo ya awali yaliyolemaza majaribio kama haya kwa kukuza vimelea ndani ya figo hizo ilikuzuwezesha vifo hizo bandia kuchunga mkojo na kupitisha pasi na kulowa.
Japo majaribio kwa binadamu hayajaidhinishwa,bila shaka matokeo haya mapya yanatoa muamko mpya katika jitihada za kuunda viungo muhimu vya mwili katika maabara ilikusaidia wagonjwa .
Daktari Takashi Yokoo na wenzake katika chuo kikuu cha utabibu cha Jikei kilichoko Tokyo walitumia mbinu hiyo kukuza figo hiyo bandia.
Profesa Chris Mason, ambaye ni mtaalamu wa maswala ya seli shina na muhadhiri katika chuo kikuu cha London, amefurahishwa sana na matokeoa haya.
''Hili ni tukio la kutia moyo sana.''
Figo hizo bandia zilifanya kazi vyema katika nguruwe na panya.
''Hata hivyo hili halimaanishi kuwa mbinu hii ya kukuza viungo itafaulu kwa binadamu.'
''Aidha kukuzwa kwa figo kunasaidia kubaini jinsi mwili unavyoondoa uchafu mwilini na ukiangalia wagonjwa wanaolazimika
'kutumia mashini ilikusafisha damu ''dialysis''mbinu hii bila shaka inatoa matumaini makubwa mno''. alisema Profesa Mason.
Watafiti wengine tayari wanafikiria kuhusu mbinu ya kukuza figo,moyo na hata mapafu.
Professa Harald Ott na wenzake wameanza kujaribu mbinu mbadala inayokuza seli shina kutoka kwa viungo vya wazee na kukuza viungo changa.
Post a Comment