MH. MAGUFULI KUFANYA MBADALA WA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA UHURU MWAKA HUU
Obeni Sefue Katibu Mkuu Kiongozi katika ofisi ya Rais wa Tanzania
amesema sherehe za Uhuru zimefutwa ili kukabiliana na kipindupindu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli, ametangaza
kufuta sherehe za Uhuru wa nchi hiyo za mwaka huu zinazofanyika disemba
tisa badala yake ameagiza siku hiyo itumike kufanya usafi kwa kila
mwananchi.Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam alisema fedha ambazo zingetumika kwenye maadhimsho ya sherehe za Uhuru mwaka huu zitaelekezwa kwenye maeneo ambayo rais ataona yanahitaji kupatiwa mahitaji sana.
"HAIKUISHIA HAPO" OLE WAO WENYE SAFARI ZA NJE YA NCHI ZISIZOELEWEKA Kuhusiana na safari za nje kwa watumishi wa umma, Balozi Sefue pia amesema rais amegiza kufanyika tathmni ya kina kwa kila anayeomba kusafiri nje ya nchi kabla hajafikiria kuomba kibali kwa katibu mkuu kiongozi.
Tangu kuingia madarakani katika awamu ya tano ya uongozi wake Rais Magufuli ametangaza kukata baadhi ya mambo ikiwemo kuzuia safari za nje zisizo za lazima pamoja hafla au tafrija mbalimbali alizosema zinapoteza fedha nyingi za walipa kodi ambazo zingetumika kutatua kero mbalimbali za wananchiWakati huo huo Balozi Ombeni Sefue amewataka watumishi wote wa Umma nchini kuanza kuvaa Beji au vitambulisho maalum vyenye majina yao mahala pa kazi ili kutoa fursa kwa wananchi kujua anahudumiwa na nani.
Post a Comment