Loading...
Advertisement

MAKALA ; BAJETI 2016/2017

[1.5MB] download video ya LULU akiwa bafuni anaoga ==> Advertisement

BAJETI CHUNGU KWA WANANCHI FUATILIA

HULKA ya falsafa ni kudadisi, kuhoji na kushangaa na nia ikiwa kusaka ukweli utakaowezesha kuondoa shaka katika jambo linaloonekana kuwa zito.

Image result for bajeti ya serikali

Nimekuwa nikiamini katika falsafa hiyo kwa muda sasa ambayo naamini imeniwezesha kutambua mambo mengi sana ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.

Kwa kutumia falsafa hiyo hiyo ya kudadisi, kushangaa na kuhoji nimejielekeza katika kusaka ukweli kuhusu ubora wa Bajeti ya 2016/17 iliyosomwa hivi karibuni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango.

Image result for bajeti ya serikali

Baada ya kuipitia nimejiridhisha pasi na shaka kwamba nina kila sababu ya kuhoji na kwa kushirikiana na wasomaji ili kubaini kama bajeti hiyo ya Magufuli itakuwa mwarobaini wa maendeleo ya serikali yake kutimiza ahadi ya kuwainua wananchi wa hali ya chini.

Sababu nyingine iliyonichagiza kutazama Bajeti ya serikali kwa kina inatokana na ukweli kwamba ndiyo inayotoa taswira ya kukamilisha jambo lolote ikiwemo muelekeo wa serikali.

Wale wanaoshabikia bajeti iliyosomwa hivi karibuni wengi wao naamini watakuwa hawajatumia falsafa ya kudadisi na kuingia kwenye mkumbo wa kushabikia kila jambo bila ya kutafakari kwa undani.

Image result for bajeti ya serikaliKama wabunge wetu wangekuwa wanatafakari mambo kwa mapana yake nakuweka vyama vyao kando na kuliweka taifa mbele naamini wasingekubali kupitisha Bajeti hiyo ninayoshawishika kusema bila kumeza maneno kwamba haifai kwa Tanzania tunayoitaka.

Kwanini haifai? Kwanza inakwenda kinyume na ndoto za Rais John Magufuli za kutaka watu wa hali ya chini kuishi kama ‘malaika’ (maisha mazuri) lakini kwa bajeti hii imewanyonga kwa kutumia kinyongeo kinachoitwa kodi.

Simaanishi kwamba ni vibaya kulipa kodi lakini kwa serikali ya Dk. Magufuli imejielekeza kuwabana watu wa hali ya chini kabisa kwa kuongeza kodi katika huduma za fedha zinazotumiwa na watu masikini za M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money.

Kuongeza kodi kwa Kampuni za simu maumivu huja kwa watumiaji ambao wengi wao ni masikini na watu wa hali ya kati, kwa kuwa pindi wanapoongezewa na wao huwaongezea watumiaji gharama za huduma.

Image result for bajeti ya serikaliTatizo jingine ninaloliona na limeanza kulalamikiwa na Halmashauri mbalimbali ni hatua ya ukusanyaji wa kodi za majengo ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikikusanywa na halmashauri, lakini sasa imeamuliwa zikusanywe na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kupelekwa Hazina. Wakati wanafanya hivyo hawakutafakari kwamba wataathiri kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri kwa sababu vyanzo vyake vikuu vya mapato ni kodi hiyo.

Kama utaratibu huo utatumika kwa fedha kukusanywa Hazina ndipo baadaye ziombwe kwa Maendeleo utacheleweshwa kama ambavyo inatokea kwa ucheleweshaji wa fedha kutoka  Serikali Kuu zinachelewa kupelekwa katika Halmashauri basi tusitegemee kuwa fedha za kodi ya majengo zitanufaisha tena Halmashauri.

Kama wangeona historia ya kuziachia Halmashauri wasingechukua uamuzi huo kwa sababu wakati kodi hiyo ilipokuwa ikikusanywa na Halmashauri na kuwasilishwa Wizara ya Ardhi ilikuwa vigumu kurejeshwa kwenye Halmashauri. Kama itafanyika hivyo inaanisha kwamba Halmashauri zitashindwa kabisa kutoa huduma kwa wananchi wake.

Tatizo jingine ninaloliona katika bajeti hiyo ya 2016/17 ni hatua ya serikali kuingiza kodi ya asilimia 5 ya kiinua mgongo cha wabunge wakati ukweli ni kwamba itaanza kutumika baada ya ukomo wa muda wa Bunge, sasa unajiuliza ni kwanini iingizwe kwenye bajeti, fedha ambayo haipo na inatarajiwa kupatikana mwaka 2020.

Ili pato hilo liweze kutumika labda serikali ingetoa mwongozo wa kusema kwamba fedha hizo zilipwe katika mwaka huu wa fedha.

Kwa suala la Tanzania ya Viwanda ambayo imekuwa ikiimbwa na Rais Magufuli ili kupunguza kama si kuondoa tatizo la ajira inaonyesha ni ngumu kutekelezeka. Ili kukamilika kwa ndoto ya rais Magufuli ilitakiwa sekta ya viwanda ilitarajiwa maendeleo ya viwanda na uzalishaji ikue kwa asilimia 11 wakati mafanikio ni ukuaji wa asilimia 6.6.

Image result for bajeti ya serikali

Bajeti imeshindwa kutueleza bayana ni kwa namna gani Tanzania itaweza kufika kwenye uchumi wa kati wa viwanda, hakuna tunapoelezwa hatua yoyote ya awali labda ya kuandaa maeneo ya kufanyia shughuli za uzalishaji wa kuwezesha viwanda, lakini ninachokishuhudia ni maneno matupu. Bajeti iliyopangwa imeendelea kutenga fedha nyingi za matumizi pamoja na kujipambanua kubana matumizi katika bajeti hii inaonyesha matumizi ya kawaida kuwa sh. 13,336,042,030,510. Wakati fedha za miradi ya maendeleo Sh. 10,511,945,288,575 pekee hivyo inamaanisha matumizi ni muhimu kuliko maendeleo.

Sitaki kuingia sana kwenye hesabu za kitabu cha Mapato ya Serikali ambayo yanaonyesha ni Sh Trilioni 22.063, huku serikali ikipanga kutumia kiasi cha Sh Trilioni 23.847 ambacho ni tofauti na mapato serikali iliyopanga kukusanya na tofauti yake inaonyesha kuwa na nakisi kubwa ya Sh. Trilioni 1.783.

Image result for kiwanja cha ndege chatoWakati tumejipangia ukuaji wa kilimo kuwa asilimia 6 kwa mwaka lakini sasa ukuaji ni asilimia 3.2 ambao ni wote kuanzia uhuru.

Suala jingine la kuhoji hapa ni kwamba kuna umuhimu gani wa kujenga kiwanja kipya cha ndege cha Chato kinamsaada gani kiuchumi kwa masilahi ya Watanzania wote? Kwanini hizo bilioni 2 zilizotengwa kwa ajili ya kuanza kufanyika upembuzi yakinifu wa ujenzi huo zisielekezwe katika kukarabati viwanja vilivyopo kwa sasa?.

Kwanini hata kabla ya mwaka mmoja wa Dk. Magufuli madarakani ajengewe kiwanja cha ndege wakati Mwalimu Julius Nyerere alikaa miaka25?

PICHA CHAFU ZA WANAFUNZI WAKIFANYA UCHAFU ZAVUJA FACEBOOK SEE PHOTOS BELOW =>AdvertisementKAMA HUJAONAILE VIDEO CHAFU YA ZARI THE BOSS LADY ILIYOVUJA BOFYA HAPO CHINI=> Advertisement

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright Storykilo | Designed By Hisia za Mwananchi
Back To Top