NI SEKUNDE 6 BAADA YA KUSHUKA KATIKA GARI LAKE POLISI MZUNGU AMFYATULIA RISASI RAIA MWEUSI MPAKA KIFO
Yamkini askari huyo alimfyatulia tineja huyo risasi 16 punde baada ya kumfumania akitoboa gurudumu la gari la polisi.
Updated 1706 GMT (0106 HKT) November 24, 2015
Kiongozi wa mashtaka wa jimbo hilo Anita Alvarez anasema kuwa video hiyo inaonesha afisa huyo akishuka kutoka kwa gari lake na kumfyatua risasi kadhaa kwa mvulana huyo ambaye alikuwa anatembea kutoka kwenye eneo la tukio.
Video hiyo iliyopigwa na kamera iliyokuwa imetundikwa kwa gari lingine la polisi inamuonesha kijana huyo McDonald akikimbia barabrani kisha alipowaona maafisa wa polisi Van Dyke na mwenzake akageuka mara moja akainua suruali yake kisha akaanza kutembea kwa kwasi kuondoka kwenye eneo la tukio.
Mara moja anavurumishwa juu na kuangushwa chini na milipuko ya risasi kadhaa.
McDonald anajaribu kuinua kichwa chake lakini risasi zaidi zinambana chini
Bila shaka hakuchukua muda wake kupeleleza hali halisi katika eneo la tukio.
Hii ndio mara ya kwanza kwa afisa anayehudumu kufunguliwa mashtaka ya kuua akikusudia.
Post a Comment